KARIBU

Jumatano, 22 Oktoba 2014

KILICHOWASHANGAZA MASHABIKI BAADA YA  MOURINHO KUZUNGUMZIA PENATI ILIYOPIGWA NA DROGBA
Meneja wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amewashangaza waandishi wahabari baada ya kusema hakufurahishwa na kitendo cha kiungo mshambuliaji Eden Hazard kumuachia mshambuliaji Didier Drogba kupiga  penati ya kwanza iliyopatikana wakati wa mchezo wa ligi ya mabingwa barani Ulaya uliochezwa usiku wa kuamkia hii leo huko jijini London nchini Uingereza.
Mourinho, amesema jukumu la kupiga penati katika kikosi chake lipo mikononi mwa Eden Hazard lakini cha kushangaza alimuona kiungo huyo kutoka nchini Ubelgiji akimpa ruhusa Drogba kutimiza jukumu ambalo halikumuhusu.
Mourinho, amesema hakufurahishwa na kitendo hicho na amewataka waandishi wa habari kutambua wazi kwamba chaguo lake katika jukumu la kupiga penati inapojitokeza katika michezo ya The Blues ni Hazard na si kwa mchezaji mwingine yoyote.
Hata hivyo meneja huyo kutoka nchini Ureno, amesema pamoja na kutofurahia maamuzi ya Hazard kumpa ruhusa Drogba kupiga penati ya kwanza katika mchezo huo, bado alijihisi kawaida kutokana na mkwaju wa mshambuliaji huyo kutoka nchini Ivory Coast kutinga nyavuni na kuizawadia bao la pili Chelsea.
.

         

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni